Pombe imeandikwa kabisa #RestInPeace na jeneza pembeni.. wako wanaoitumia kabisa !! By j.twice
Kenya imetajwa kwenye Top Ten ya nchi Tajiri Afrika 2015, hiyo ni good news.. Zimebaki wiki kama tatu hivi ili tushuhudie Rais wa Marekani, Barrack Obama anatembelea nchi hiyo, hiyo ni good news.. lakini ziko story upande wa pili wa shilingi pia.
Kama wewe ni mtazamaji wa Taarifa za Habari kwenye TV za Kenya itakuwa umeshuhudia pia majanga ya pombe za kienyeji, wapo wanaofariki, wengine wanajikuta hali mbaya mpaka wanalazwa Hospitali, lakini bado kuna wengine wanaendelea kutumia vilevile!!
Huyu ni mmoja ya watu waliozidiwa na kujikuta hawana hata nguvu ya kuinuka kutembea.
Moja ya vitu vilivyonishtua ni hii kukutana na chupa ya Pombe ambayo wanasema hata haijasajiliwa na inauzwa kama kawaida. jina lake je? >> Inaitwa ‘Rest in Peace Premium Vodka‘ na kuna picha ya Jeneza kabisa kwa chini yake.


No comments:
Post a Comment